Azam na Yanga zitakutana na hawa kwenye michuano ya CAF.



Timu zitakazoiwakilisha Tanznaia kwenye mashindano ya kimataifa kwa ngazi ya vila hii leo zimefahamu wapinzani wake katika michuano hiyo kwa msimu wa mwaka 2014 / 2015 baada ya ratiba ya michuano ya Klabu Bingwa barani Afrika na kombe la shirikisho kupangwa huko Cairo.
Ratiba hiyo inaonyesha kuwa mabingwa wa Tanzania Azam Fc wamepangwa kucheza na Al Mereikh kwenye raundi ya kwanza ya ligi ya mbingwa huku wawakilishi toka Zanzibar KMKM wakicheza na timu nyingine toka Sudan ya Al Hilal .

Azam wataanzia nyumbani dhidi ya Al Merreikh 

Timu nyingine toka Tanzania Yanga itacheza na timu ya jeshi la ulinzi ya Botswana BDF huku Polisi ya huko Zanzibar ikicheza na CF Mounana ya nchini Gabon .
Ratiba inaonyesha kuwa michezo ya kwanza itafanyika kati ya tarehe 13 , 14 na 15 mwezi wa pili mwakani huku mechi za marudiano zikifanyika wiki mbili baadae yaani tarehe 26 , 27 mwezi wa pili na tarehe 1 mwezi machi .

Azam fc na Yanga zinatarajia kuanzia nyumbani huku KMKM wakianza ugenini huko Omdurman nchini Sudan .


Mchezo kati ya Azam Fc na Al Merreikh utakuwa maalum kwa beki mpya wa timu hiyo ya Tanzania Serge Paschal Wawa ambaye atakuwa na nafasi ya kukabiliana na timu yake ya zamani kwa mara ya kwanza tangu aliposajiliwa toka Al Mereikh wiki chache zilizopita .

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini