MVUA ILIYONYESHA JANA JIJINI DAR YASABABISHA VIFO

Mvua iliyonyesha jijini Dar es salam imeleta balaa baada ya kuua watu wawili katika maeneo tofauti ya jiji hilo likiwemo tukio la mtoto wa miaka minne kufa baada ya kuzidiwa na maji yaliyoingia ndani ya nyumba wakati akiwa amelala.
Kwa mujibu wa Taarifa ya kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar Camilius Wambura alisema matukio hayo yalitokea jana mchana kwenye maeneo mawili tofauti.
Tukio la kwanza lilitokea eneo la Tandale ambapo mtoto Nasma Ramadhani akiwa amelala ndani ya nyumba yao maji ya mvua yaliingia ndanina kumzidia nguvu hadi kufariki na mwingine bibi kizee kufariki eneo la Mwananyamala aliyeangukiwa kichwani na ukuta wa nyumba yake na kumsababishia mauti.
Wambura alisema madhara mengine ni maji kujaa kwenye ameneo mbalimbali ikiwemo Mikocheni zilizopo ofisi za Tanesco,Kinondoni jirani na TMJ hivyo kuleta usumbufu wa Magari na watukuvuka eneo hilo.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini