Kiwanda cha juisi chafungwa, picha ya uzalishaji inajieleza...

Baadhi ya juisi hizo zikizalishwa

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) imekifungia kiwanda cha Devideic cha mjini Morogoro kwa muda usiojulikana kuendelea na uzalishaji wa juice aina ya Into baada ya vipimo vya kimaabara vya Shirika hilo kubaini kiwango cha sukari inayotumika haifai kwa binadamu pamoja na mazingira ya uchafu.

Matumizi hayo ya sukari isiyofaa na mazingira hayo ya uchafu yanahatarisha usalama wa afya za walaji wengi yakiwemo makundi ya rika mbalimbali na watoto.
Kufungiwa kwa Kiwanda hicho kuendelea kuzalisha bidhaa ya aina hiyo kulifanyika jana ( Des 29),baada ya maofisa wa TBS kutoka makao makuu Jijini Dar es Salaam , kufanya ukaguzi wa kushitukiza katika kiwanda hicho kilichopo eneo la Kihonda, Maniapaa ya Morogoro.

Ukaguzi hu wa kushitukiza ulifanyika chini ya ulinzi wa Polisi na baada ya kufika kiwandani hapo, wafanyakazi kadhaa walikutwa wakijaza juici iliyojazwa kwenye matenki kwa kupitia mabomba yaliyowekwa kiko tofauti na utaratibu wa kiuzalishaji.

Ofisa Viwango na Mkaguzi wa TBS, Lawrence Chenge, baada ya kujilizisha na ukaguzi wake katika maeneo ya stoo, mitambo, matenki , mifumo ya maji na aina ya viwango vinavyohitajika ndani ya juice hiyo , ulibani kuwa na kasoro nyingi na kukosekana kwa aina viwango vinavyohitajika kuihalalisha kuwa na ubora halisi kwa watumiaji.

“ Tumefanya ukaguzi mara kadhaa na mara zote tumetoa kutoa maelekezo maeneo ya sehemu ya kurekebishwa ...lakini hadi sasa hawajafanya juhudi zozote “ alisema na kuongeza
“ ...Tumepima tena juici hii ya Into kwenye maabara zetu na kugundulika kuna kasoro nyingi ya kukosekana viwango muhimu vinavyotakiwa kwenye bidhaa hii na kwa maana hii haijakidhi viwango na haifai kwa matumizi ya binadamu na wengi wakiwa ni watoto “ alisema.

Kutokana na mapungufu hayo, TBS imechukua jukumu la kukifungia kiwanda hicho kisiendelee na uzalishaji wake katika bidhaa hiyo hadi pale uongozi wa kiwanda utakaporekebisha yale yaliyobainika kwenye ripoti kimaabara nay a kiukaguzi na kukaguliwa tena kabla ya kuruhusiwa.

Wakati kiwanda hicho kinafungiwa kuendelea na uzalishaji wa aina hiyo ya juici, tayari katoni 50 zilikutwa zimezalishwa na nyingine kurundikwa kwenye madishi makubwa.

Naye Ofisa Uhusiano wa TBS, Roida Andusamile, alisema kuwa Shirika hilo lina maabara za kisasa na kuwa na uhakika wa matokeo ya majibu ya upimaji wa sambuli ya juici hiyo inayozalishwa na kiwanda hiyo.

Kwa mujibu wa Ofisa huyo, kutokana na ubora wa maabara hizo,matokeo ya majibu ya viwango chake hata upimaji huo ukipelekwa nje ya nchi hakutakuwepo na utofauti wa majibu.

Hivyo alisema, uchunguzi wa kimaabara na matokeo yake ni kwamba juichi hiyo ina uchafu na inatumia ‘sweetner’ kinyume na kiwango kinavyotakiwa na hivyo kuwa na madhara kwa binadamu.

Mbali na hayo ,alisema bidhaa iliyopo sokoni ‘ madukani’ itaondolewa na kutakiwa isiendelee kuuziwa wateja kutokana na mapungufu yaliyomo kwenye juici hiyo.

Kwa mujibu wa Ofisa Uhusiano huyo , kiwanda hicho kimeanzishwa kihalali kupitia mfumo wa viwanda vidogo vodogo vya wajasiliamali chini ya mpango ulioanzishwa na Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) mwaka 2011 na kilipewa alama ya TBS kwa masharti ya kuzalisha bidhaa zenye viwango vya ubora kwa mujibu wa sheria na pale kinapokwenda kinyume kitafungiwa kama vinavyofungiwa viwanda vingine vikubwa.

Kwa upande wake Meneja wa Uzalishaji wa Kiwanda hicho, Thadeus Ngonyani, licha ya kujitetea kuwa wanazingatia viwango vya ubora ,alijikuta akilemewa na maswali kuliko majibu huku akitoa lamawa kuwa huo ni uonevu na kuwa ni vita vya kibiashara kwa kukifungia kiwanda chake.

Hata hivyo akilishindwa kujitetea pale alipotakiwa kuanisha aina ya viwango ‘ Ingredients’ iliyomo kwenye juici hiyo aina ya Into na pia kuendelea kujaza juici kwa mfumo wa njia ya kawaida wakati ulipokatika umeme.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini