UMEISIKIA HII YA WALE WATUHUMIWA WALIOMUUA DKT SENGONDO MVUNGI?

Washtakiwa 11 wa kesi ya mauaji ya kukusudia ya aliyekua mjumbe wa tume ya mabadiliko  ya Katiba,Dk Sengondo Mvungi jana waligoma kwa muda kuondoka kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu wakishinikizwa kuelezwa lilipo jalada la kesi yao na hatua ilipofia.
Hilo lilitokea jana saa nne asubuhi ,muda mfupi  baada ya wakili wa serikali,Peter Njikekumweleza Hakimu Hellen Liwa kuwa kesi hiyo ilifika mbele yake kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi wake bado haujakamilika na kuomba ipangwe tarehe nyingine.
Mshtakiwa Masunga Makenza alidai hafahamu sheria ,kesi hiyo ni ya muda mrefu na akahoji jalada likienda kwa DPP linatakiwa kukaa kwa muda gani.
Makenza alidai kuwa kesi hiyo ni ya kubambikiwa na kwamba ingekuwa halisi,upande wa mashtaka ungekuwa umekwishakamilisha upelelezi na kwamba wapotayari kushtakiwa ila kama upande wa mashtaka umeshindwa kukamilisha upelelezi mahakama iwaachie huru na ikikamilisha iwakamate tena.

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini