Afande Sele aonesha mjengo alioujenga kupitia pesa ya muziki (Picha)



Msanii mkongwe wa Hip Hop kutoka Morogoro, Afande Sele ameonesha nyumba aliyoijenga nje ya mji wa Morogoro kupitia pesa za muziki. Rapa huyo ambaye mwaka 2015 aligombea ubunge katika jimbo la Morogoro mjini kupitia ACT, ameiambia Bongo5 kuwa anakamilisha mjengo wake na kurudi kijijini. “Muziki ulishatupaga heshima.
Hii pia ndio culture yetu rasta hata Babu Burning Spear alirudi shamba. Huu ni witoAmeongeza,“Sijaacha muziki ila muziki ndio umeniacha. Muziki nitafanya kama hobby tu pale nikipata maono poa ambayo itabidi nifikishe ujumbe kwa watu nitaandika nyimbo. Ila pia huu uwe mfano Kilimo kinalisha dunia.”

ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini