Rais MAGUFULI Ampinga Balozi SEFUE Live!

Katika hali inayoonyesha utendaji wa Rais Magufuli ni wa ufuatiliaji wa karibu, juzi alifuta utaratibu wa protokali uliokuwa umetangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue na kuagiza itumike njia yake, wakati wa hafla ya kuapisha Makatibu Wakuu na Makatibu Wasaidizi wapya wa wizara mbalimbali aliowateua hivi karibuni.

Makatibu wakuu na manaibu wao walifika Ikulu kwa ajili ya shughuli ya kuapishwa kushika nafasi zao na baadaye kusaini kiapo cha uadilifu kilichoongozwa na Naibu Kamishna wa Maadili, Waziri Kipacha.

Mara baada ya Kamishna huyo kusoma kiapo hicho kwa niaba ya makatibu wakuu na manaibu hao, Katibu Mkuu Kiongozi aliwataka makatibu wakuu na manaibu hao kila mmoja asaini katika hati aliyopewa.

Utaratibu huo uliotangazwa na Balozi Sefue ulionekana kutomridhisha Rais Magufuli ambaye katika hali ambayo haikutarajiwa, aliinuka kutoka sehemu aliyokuwa amekaa na kutoa utaratibu tofauti.


“Hapana huwezi kula kiapo kwa niaba ya mtu mwingine wakati wenyewe wote wapo hapa, kila mmoja aape kwa mdomo wake mwenyewe na kusaini," alisema Rais Magufuli na kutoa angalizo:
"Kama kuna mmoja wao hajakubalina na kifungu kwenye hati hii tutajuaje?

“Kama yupo Katibu Mkuu au Naibu Katibu Mkuu anayeona kuwa hataweza kutekeleza mojawapo ya vifungu vilichopo katika hati hiyo ya maadili akae pembeni atuache wengine tuendelee.”

ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini