Hii ni mipango mingine ya meneja wa Chelsea Guus Hiddink kwa klabu yake…







Pamoja na mabingwa watetezi wa ligi kuu ya England Chelsea kupoteza matumaini ya kutwaa ubingwa kwa mara nyingine lakini kocha wao mpya Guus Hiddink ana mipango mingine ya ushindi.

Baada ya ushindi wa jana wa mabao 3-0 Hiddink amesema klabu yake hiyo inaweza kumaliza ligi hiyo ikiwa katika nafasi nne bora za juu mwishoni mwa msimu huu.

Klabu hiyo ya Stamford Bridge imeenda mechi nne bila kufungwa, kwa mara ya kwanza msimu huu, na kupanda hadi nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi.

Hata hivyo, bado wanapungukiwa na alama 13 kuweza kufuzu kcheza Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Alisema ligi ni ngumu lakini pia ni rahisi kushinda hivyo watapambana kuhakikisha wanashika nafasi za juu.

Hiddink alichukua nafasi ya kuifundisha timu hiyo kwa muda baada ya kocha wa awali Jose Mourihno kuondolewa kutokana na mwenendo mbaya wa timu.


ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini