Lukuvi: Tunataka nyumba nafuu za ukweli

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuandaa mpango wa haraka wa mradi wa kujenga nyumba za gharama nafuu utakaokuwa na ukweli wa unafuu huo Alitoa agizo hilo jana alipotembelea ofisi za shirika hilo mkoani hapa.
Alisema kuanzia sasa, NHC lazima ibuni mbinu rahisi za kujenga nyumba bora ambazo zitauzwa kwa gharama nafuu ya ukweli kuliko zinazouzwa sasa ambazo alisema wananchi wengi wanashindwa kuzinunua kwa sababu bei yake ni kubwa. 
‘‘Acheni kuilalamikia Serikali kwa kuchukua fedha za Ongezeko la Thamani (VAT) kwenu kwamba ndiyo inayoongeza gharama za ujenzi, fanyeni utafiti wa namna ya kuanza kujenga nyumba bora na za gharama nafuu kiukwelikweli ambazo mnaweza kujenga mijini na hata kwenye miji midogo midogo vijijini’’ alisema.
 Lukuvi alisema Watanzania wamechoka kusikia taasisi zinatangaza kwamba zinajenga nyumba za kuuza kwa gharama ndogo wakati bei inakuwa kubwa sawa na nyumba za kuuza kibiashara. Awali, 
Meneja wa NHC Mkoa wa Mbeya unaojumuisha na Mkoa wa Njombe, Juma Kyaramba alimweleza waziri Lukuvi kwamba wanaendelea na ujenzi wa nyumba za kuuza wilayani Mbarali na Makete ambazo zitauzwa kwa bei nafuu. Kyaramba alisema NHC Mbeya ambayo ina majengo 42 yenye maeneo zaidi ya 200 ya kupangisha, ilikusanya zaidi ya Sh1 bilioni mwaka jana na mwaka huu inatarajia kukusanya 1.3 
bilionii. Pia, waziri Lukuvi alikagua madeni ya wateja ambayo yanafikia Sh43 milioni kubwa likiwa la Sh30.5 milioni la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Sh9.9 deni la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Sh3 milioni inazoidai Hospitali ya Rufaa Mbeya


ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini