Ditto ataja sababu za wasanii wapya kupotea

Msanii na mtunzi wa nyimbo, Lameck Ditto amesema wasanii wengi wachanga wanashindwa kufanikiwa kutokana na woga pamoja na kutokuwa wabunifu kwa kukopi kazi za wasanii waliowakuta kwenye game. Ditto ambaye pia kwa sasa amejikita kwenye kilimo cha biashara, amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio kuwa, 
kama wasanii wangeamini wanachofanya pamoja na kuwa wabunifu, wangefanikiwa. “Kitu kikubwa wanashindwa kuwa tofauti na wengine,” alisema. “Mimi naona vijana wengi wapo hivyo, hawana ubunifu yaani kama ni waoga waoga hawaamini wanachokifanya ndio maana wanaiga kile wanachokiona. Mimi nawashauri wajitahidi kuonyesha utofauti,
 wafanye kazi kwa bidii hakuna kitu cha ajabu wote wamepitia huko huko,” alisema.

ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini