Tutegemee Kumuona CHICHARITO Arsenal January? Alichokisema Mkurugenzi wa Bayer Leverkusen Hiki Hapa

Mshambuliaji wa kimataifa wa Mexico ambaye amewahi kuichezea klabu ya Man United kwa miaka kadhaa Javier Hernandez Chicharito kabla ya mwaka 2015 kuamua kujiunga na klabu ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani, amekuwa akihusishwa kuhitajika na klabu ya Arsenal ya Uingereza. 

January 3 mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo Rudi Voller ameongelea uwezekano wa mchezaji huo kuondoka ndani ya Leverkusen ni mdogo sana hususani ukizingatia wapo katikati ya msimu, hivyo ni ngumu kwa wao kumuacha aondoke. Jibu hilo linakuwa pigo kwa Arsenal ambao wanatajwa kuwa walikuwa na imani ya kumpata.


“Chicharito ana nafasi kubwa sana ndani ya kikosi chetu, hususani kwa aina yake ya ushambuliaji na ndio maana tukamsajili katika timu yetu, ndio kwanza tupo katikati ya msimu na kila kitu kinaenda sawa ni rahisi kukataa ofa za vilabu vingine” >>> Rudi Voller 

Kauli ya Rudi Voller inalenga kuvikatisha tamaa vilabu vya Ulaya ambavyo vimekuwa vikivutiwa na huduma ya mmexico huyo. Chachiroto hadi sasa amefunga magoli 11 katika michezo 1 aliyocheza katika Ligi Kuu Ujerumani.

ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini