Matapeli 15 wa viwanja wadakwa



Zaidi ya watu 15 wamekamatwa kwa tuhuma za uvamizi na uuzaji wa viwanja vya watu katika Mtaa wa Kulangwa, Kata ya Goba Manispaa ya Kinondoni katika kipindi cha wiki moja. Kwa sasa watu hao wanashikiliwa na Polisi katika Kituo cha Wazo kwa tuhuma za kujihusisha na utapeli wa uuzaji wa viwanja vya watu vikiwamo vilivyotengwa na manispaa kwa shughuli za kijamii. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kulangwa,

 Shafii Mkwepu alisema vitendo hivyo vimekithiri katika mtaa huo. Mkwepu alidai kuwa matapeli hao ambao wanamtandao mkubwa, wamekuwa wakiuza viwanja mbalimbali vya wananchi kwa kutumia mihuri feki ya ofisi ya serikali ya mtaa huo. “Matapeli hawa hutangaza kuwa kuna viwanja vinauzwa na Manispaa, hivyo watu wengi wamekuwa wakitoka maeneo mbalimbali na kuja katika mtaa wa Kulangwa kwa ajili ya kupimiwa viwanja hivyo, hapo ndipo huwalizwa na matapeli hao,”

 alidai Mkwepu na kuongeza: “Kutokana na tatizo hilo, wananchi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama, tumefanikiwa kuwakamata watu 15 ambao wanasadikiwa kuhusika na utapeli huu.” Alisema inadaiwa watu hao wamejipatia fedha zaidi ya Sh80 milioni baada ya kuuza viwanja hivyo. Alisema hiyo ni mara ya pili kwa watu hao kufanya utapeli huo. 

“Tunalaani kitendo hiki na ninawahakikishia wananchi kuwa viwanja vyao vitakuwa salama na mpaka sasa Manispaa haijatoa taarifa kuhusu uuzaji wa viwanja hivyo ila wananchi nao wanatakiwa kuwa makini na matapeli hao,” alisema. Alisema wiki iliyopita matapeli hao walivamia kiwanja cha shule ya Oktavian Tema chenye ukubwa wa heka nne walichotaka kukiuza, bahati nzuri hawakufanikiwa baada ya Serikali ya Mtaa kupata taarifa na kuweka ulinzi. Hata hivyo, itakubukwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda alishawahi kusema kuwa wilaya yake inakabiliwa na changamoto ya migog


ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

Popular posts from this blog

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama

Walimu wadaiwa kuacha vipindi kukimbilia kufanya kazi migodini