Petit Man Amuanika Mrithi wa Dada wa DIAMOND, Esma!
Mpambe wa staa wa Filamu Bongo, Wema Sepetu, Hamadi Manungwa ‘Petit Man’, juzikati alimuanika rasmi mrithi wa aliyekuwa mkewe, Esma Abdul ‘Esma Platnumz’ baada ya hivi karibuni kuingia kwenye mgogoro wa ndoa.
Baada ya gazeti hili kuanika habari ya kuvunjika kwa ndoa hiyo wiki iliyopita huku Wema akitajwa kuwa chanzo ambapo yalizuka mambo mengi mpaka watu kupelekana polisi, hivi karibuni Petit Man alimuanika mwanamke mwingine akidai ndiye wa kuchukua nafasi ya Esma.
Esma kwa upande wake alisema anachosubiri ni talaka yake tu kwani ameshachukua baadhi ya vitu vyake kwenye nyumba waliyokuwa wakiishi na Petit Man.