WANAFUNZI 459 WA DARASA LA KWANZA WANASOMEA KWENYE DARASA MOJA JIJINI DAR
Hali hiyo ya wanafunzi kusoma katika
darasa moja na wengine chini ya miti inayozunguka shule hiyo,
inachangiwa na upungufu wa majengo ya shule hiyo ambayo ina vyumba saba
vya madarasa huku ikiwa na zaidi ya wanafunzi 2,038.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Saku, Salome Munisi alisema
shule yake inakabiliwa na changamoto kubwa ya uchache wa madarasa
pamoja na wingi wa wanafunzi kuliko uwezo wa vyumba vya madarasa
walivyonavyo.
Munisi alisema idadi ya wanafunzi
walioandikishwa darasa la kwanza mwaka huu ni kubwa kuliko darasa la
pili ambalo lina wanafunzi 436, wakiwamo wanaume 217 na wasichana 219.
“Kipindi
cha mitihani inabidi wanafunzi wafanye mtihani chini ya mti kwa sababu
wako wengi darasani, huwezi mwalimu kuwapa mtihani watatizamiana na
itakuwa ngumu kupima kiwango cha elimu kwa wanafunzi kwa sababu watajaza
majibu yote yanayofanana“:- Munisi.